Saturday, January 26, 2013

PASTOR FRANK JULIUS akiwa anahubiri studio za BREEZE FM Tanga katika kipind cha African Gospel Time



PASTOR FRANK JULIUS WA SHILO CHURCH AKIWA STUDIO ZA BREEZE FM Tanga Akiwa anahubiri neno la mungu..

Kama ndo kwanza unajiuliza wewe mkazi wa Tanga unajiuliza kanisa  la shilo church linalotumiwa na mungu kwa hali ya juu sana kupitia mtumish wa mungu Pastor Frank Julius kanisa lipo Majestic linaangaliana na shule ya old Tanga karibu uabudu na shilo church


Thursday, January 24, 2013

AIC KAMBARAGE SHINYANGA YAMPOTEZA MWENZAO

AIC KAMBARAGE SHINYANGA YAPOTEZA MWIMBAJI WAO
Marehemu Jane katikati aliyekumbatia kitabu akiwa na waimbaji wenzake.

 Kwaya ndugu ya AIC shinyanga wana wa Ng'ang'ania iitwayo AIC Kambarage Choir siku ya jana jioni imempoteza mmoja wa waimbaji wake mahiiri wa sauti ya kwanza na ya pili aitwaye Jane ambaye alikuwa amelazwa katika hospitali ya mkoa wa Shinyanga kwa matibabu.

Worship  With MARANATHA CRISTIAN MINISTRY Arusha

Karibu uabudu na MARANATHA CHURCH ARUSHA MIANZIN kanisa linaloongozwa na mtumish wa mungu ERICK MUKWENDA kama mbeba maono wa huduma hiyo
      Ibada zao zinakuwa hivi:  jumapili ibada mbili
                                                Ya kwanza inaanza 7:00 _ 9:30
                                                       Ya pili                9:30_ 11:30
                                            juma tano( bible study) 3:30 _6:00
         welcome  MARANATHA CRISTIAN CENTRE ARUSHA KWA IBADA NZURI UKUTANE NA BWANA KUPITIA IBADA NZURI PAMOJA NA KUSIFU NA KUABUDU KATIKA ROHO NA KWELI KUPITIA PRAISE AND WORSHIP TEAM NZURI.

"UPO HAPA" Albam mpya ya John Lisu  atkayoizundua hivi karibuni na kusindikizwa na waimbaji wengineo wengi.

Hiv karibuni mwimbaji aliyefanya vizuri na mwenye historia kubwa  hapa Tanzania katika Muzik wa Gospel
na Wakwanza kufanya live Recording ya Dvd JEHOVA YU HAI iliyobeba picha na uhalisia na maana ya kusifu na kuabudu kupitia nyimbo zilizomo ndani ya albamu hiyo iliyokuwa ya kwanza .

sasa basi hiv karibun John Lisu atazindua Albamu yake ingine iliyobeba jina la UPO HAPA atakayoizundulia
CCC Upanga Dar es salaam tareh 9/02/2013 ambapo atasindikizwa na waimbaji wengi wa muziki wa Gospel na wanaofanya vizuri pia kama Pastor Safari,Cosmas chidumule,Glorious celebration,Bomby johnson, The voice pamoja na Next level kuanzia saa nane mchana kama wewe ni mkazi wa Dar es salaam ama mkoani bado unanafasi ya kuwahi usikose kushiriki baraka hiyo.

J.SISTERS IN GOSPEL MIKAKATI AMBAYO WAPO NAYO KWA 2013 JE WATAKA KUJUA NIN WANAKUANDALIA  MSIMU HUU.

  Unaweza ukasema wapo kimya sana labda baada ya uzinduzi wao wa albamu ya TAKE A VICTORY AUDIO ambapo video ilikuwa bado lakin ilienda kufanyiwa huko nchi za wenzetu kwa sasa HIGHGOSPEL imethibitisha kama ipo njian na ipo kitofauti sio kama wengi walivyozoea kuona video tofauti tofauti ambazo zinakuwa zinafanyika hapa nyumbani kwetu kwahivyo kaa tayari kwa TAKE A VICTORY VIDEO

     GLORIOUS  CELEBRATION WAKIWA KATIKA POZI

Unapoongelea vikundi ambavyo vinavyofanya vizuri hapa tanzania glorious ni mojawapo kutokana na kazi yao lakin vilevile albamu ingine mpya ipo jikon hivi karibuni itakuwa imeachiliwa baada ya HIGHGOSPEL kufanya mahojiano na kiongozi wa band hiyo Emanueli Mabisa
   "tunatarajia makubwa katika albamu yetu mpya ambayo hivi karibuni tutaichia albamu ingine mpya na tunamuamini mungu atafanya kupitia albamu hii wengi watabarikiwa na watafunguliwa wakiwa wanasikiliza nyimbo hizi mpya na mungu awabariki"   Hayo aliyasema Emanuel mabisa

JE WAJUA...


KIJANA  MWENYE  SAUTI YA  KUVUTIA  NA ALIYETIKISA KATIKA NYIMBO MPYA KUTOKA GLORIOUS CELEBRATION..PAUL

Paul akiwa katika moja ya ibada ambayo alikuwa na glorious celebration group linalofanya vizuri katika
tasnia ya Muziki wa Gospel Tanzania na anamatarajio makubwa ana ndoto nying sana kupitia kipaji chake.